TUME YAUNDWA KUCHUNGUZA MITAALA ILIYO WASILISHWA NA WAZIRI KAWAMBWA

 











Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, kuwasilisha jana nakala za mitaala bungeni kama alivyoahidi wiki iliyopita, hofu ya kujiuzulu Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia imegubika NCCR-Mageuzi.

Waziri Kawambwa aliwasilisha mitaala ya elimu ya awali, msingi na sekondari ya mwaka 2005 bungeni, kabla ya kuanza kipindi cha maswali na majibu kama alivyoahidi Januari 31.
Muda mfupi baada ya hilo kufanyika bungeni Dodoma na Bunge kuamua kuihakiki kama haijachakachuliwa, hofu ilitanda NCCR-Mageuzi, kutokana na kiapo cha Mbatia kwamba ikiwasilishwa, atajiuzulu ubunge.
Kutokana na hofu hiyo, Katibu wa Uhusiano na Uenezi Taifa, Kitengo cha Vijana wa NCCR-Mageuzi, Deogratius Kisandu, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akielezea kutokubaliana na hatua ya Mbatia kujiuzulu.
Kuwasilishwa kwa mitaala hiyo, kulitokana na hoja binafsi ya Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi akidai kwamba Serikali haina mitaala na ndiyo maana elimu nchini inaendeshwa kwa udhaifu.
Mbatia aliitaka Serikali iwasilishe mitaala hiyo Januari 31 na kuahidi kuwa kama ingewasilishwa, angekuwa tayari kujiuzulu. Kutokana na madai hayo yaliyoendana na kiapo, Naibu Spika, Job Ndugai, alimwagiza Dk Kawambwa kuileta mitaala hiyo bungeni jana.
Hata hivyo, kabla ya kuwasilishwa kwa mitaala hiyo, Mbatia alifanya mkutano na waandishi wa habari bungeni na kusema kwa kuwa Serikali ilishindwa kuwasilisha mitaala Januari 31, iliyoletwa jana, itakuwa imechakachuliwa.
Kamati ya Bunge Kutokana na kauli hizo za Mbatia, baada ya Dk Kawambwa kuwasilisha mitaala hiyo kama alivyoahidi, Ndugai aliunda Kamati ya watu sita kuichunguza kama ni halisi au imechakachuliwa.
Naibu Spika alisema maadam mitaala hiyo iliwasilishwa mezani kwake, jukumu la kujua uhalisia si kazi ya Mbunge, bali ya Bunge na kwa mantiki hiyo, akaunda Kamati kuangalia uhalisia wake.
Alitaja wajumbe sita wa Kamati hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii za Bunge, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu, Margaret Sitta (CCM) na Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa (CCM).
Wengine ni Mbunge wa Chwaka, Yahya Kassim Yahya (CCM); Mbunge wa Viti Maalumu, Bernadetha Mshashu (CCM); Mbunge wa Karatu, Israel Natse (Chadema) na Mbunge wa Gando, Khalif Suleiman Khalifa (CUF).
Pamoja na kuunda Kamati, Naibu Spika alimruhusu Mbatia kushirikiana na Kamati hiyo pamoja na watendaji kutoka serikalini, ili kuhakiki mitaala kama imechakachuliwa au la.
Alisema kama Kamati hiyo itabaini mitaala ni halisi, wataigawa kwa wabunge kwa ajili ya matumizi yao. Hofu NCCR Pamoja na kuwa Mbatia hajazungumzia kujiuzulu kwake, wala Bunge halijamtaka achukue hatua kutekeleza kiapo hicho, Kisandu katika taarifa yake alisema:
“Sisi vijana wa NCCR-Mageuzi tunasema hatutakubali Mwenyekiti wetu ajiuzulu ubunge, eti kwa sababu mitaala imepatikana, kwani Serikali ilikuwa wapi kuitoa tangu miaka yote hiyo mpaka Mbatia ‘akakomalia’ ndipo ipatikane? “Hajiuzulu mtu hapo, kwa nini hawakupeleka siku ile aliyotaka Mbatia? Je, kama wamekwenda kuitengeneza, kuna uhalali gani wa Mbatia kujiuzulu?
Tuamke Watanzania,” alieleza Kisandu. Alisisitiza kuwa kama Serikali ingepeleka mitaala siku ambayo Mbatia aliiomba, wangekubaliana naye ajiuzulu, lakini kwa kuwa muda umepita, hawakubali ajiuzulu.
“Hakuna haja ya kujiuzulu. Waulize walimu na wakufunzi wao na maprofesa wao kama wamewahi kuiona pamoja na kuwa na kozi inayohusu mitaala vyuoni, hebu nenda shuleni na vyuoni kama utaiona.
“Sasa Mbatia kafungua ukurasa mpya, shinikizo lake limewezesha hata wadau waone mitaala ya elimu ya Tanzania. Rai yangu magazeti yaichapishe ili nasi tufaidi yaliyomo,” alishauri.
SOURCE:-HABARI LEO

Comments