Wolper ambaye sasa anafahamika kwa jina la Ilham alisema, ni kweli alibadili dini baada ya kuchumbiwa na Dallas lakini atakuwa anamchezea Mungu kama ataamua kurudi kwenye Ukristo baada ya uchumba kuvunjika.
“Mimi nitabaki kuwa Muislam hadi kifo, siwezi kurudi kwenye Ukristo kwani nilikuwa nikiupenda Uislam.
Akitokea mwanaume Muislam akataka kunioa niko tayari na hata akija Mkristo pia ila nitaendelea kuwa Muislam,” alisema Wolper.
Wolper alibadili dini siku chache zilizopita baada ya kuingia kwenye uhusiano na Dallas lakini hivi karibuni kulikuwa na madai kwamba amerudi kwenye Ukristo, jambo ambalo amelikanusha.
Comments
Post a Comment