SHILOLE, SAJENTI WAKWIDANA CHOONI!

WASANII wa filamu za Kibongo, Zuwena Muhammed ‘Shilole’ na Husna Idd ‘Sajent’ hivi karibuni walizinguana na kufikia hatua ya kukwidana katika choo kilichopo ndani ya viwanja vya Leaders Club jijini Dar.
Chanzo chetu kilichokuwa katika eneo la tukio kilidai kuwa, kisa cha wawili hao kukwidana kilianzia kwenye kikao cha kuchagua uongozi mpya wa Bongo Movies.

“Katika kikao hicho, walianza kujadili mwenendo wa wasanii ambapo ilifika wakati Shilole na Sajenti walitofautiana, Shilole alipokwenda chooni, Sajenti alimfuata na huko ndiko kuliibuka timbwili,” kilidai chanzo hicho.
Katika kujua ukweli wa tukio hilo, Ijumaa Wikienda liliwatafuta wahusika ambapo Shilole alipopatikana alisema: “Zile zilikuwa ni tofauti za kawaida tu kama mnavyoweza kutofautiana nyie kazini, kwa sasa tuko sawa.”

 

Comments