RAIS SHEIN AMTIMUA WAZIRI WAKE

RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein amefuta uteuzi wa Mansoor Yussuf Himid kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, na hivyo kupoteza wadhifa wake wa Waziri asiye na Wizara Maalumu.

 
Katika uteuzi alioufanya juzi wa mawaziri, manaibu mawaziri na makatibu wakuu, Dk Shein kwa kutumia uwezo aliopewa chini ya Kifungu 48(a) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, alifuta rasmi uteuzi huo wa Himid.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Dk Abdulhamid Yahya Mzee ilieleza kuwa Dk Shein pia amemteua Shawana Bukheti Hassan kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi kumbadili Mwakilishi huyo wa Kiembesamaki. Uteuzi huo ulianza juzi.
Hata hivyo, Ikulu ya Zanzibar haikueleza sababu za kufutwa uteuzi wa Himid ambaye aliomba kujiuzulu pia nafasi ya Waziri wa Kilimo na Maliasili miezi minne iliyopita.
Katika siku za hivi karibuni, Himid ambaye ni Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Uchumi na Fedha Zanzibar, ametangaza rasmi kuwa muumini wa Muungano wa mkataba ambao unakwenda kinyume cha Sera za chama chake kinachotetea na kulinda Muungano wa Serikali mbili.
Aidha, Dk Shein kwa kutumia uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 47 cha Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 amefanya uteuzi wa naibu mawaziri kwa kumteua Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili, Mtumwa Kheir Mbarak na pia Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi anakuwa Mohammed Said Mohamed.
Katika uteuzi huo, Dk Shein pia ameteua makatibu wakuu ambapo Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano anakuwa Dk Juma Malik Akili wakati aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk Vuai Iddi Lila atapangiwa kazi nyingine.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Makazi, Maji na Nishati ni Ali Khalil Mirza wakati aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mwalim Ali Mwalim atapangiwa kazi nyingine.
Kwa upande wa naibu makatibu wakuu, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano ni Tahir Abdulla wakati aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Msanif Haji Mussa atapangiwa kazi nyingine.
Aidha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Makazi, Maji na Nishati ni Mustafa Aboud Jumbe ambaye anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Abdulla aliyekwenda Miundombinu na Mawasiliano. Pia, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anaeshughulikia Idara Maalumu za SMZ, Julius Nalimy Maziku anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Juma Abdulla Juma aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari hivi karibuni.
Pamoja na hao, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo), Juma Ameir Hafidh anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Abdi Khamis Faki aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Bodi ya Mapato (ZRB) hivi karibuni.
Mwingine ni Saleh Ramadhan Ferouz kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii anayechukua nafasi iliyoachwa wazi naMirza aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Makazi, Maji na Nishati.
Aidha, Mussa Haji Ali ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa

Comments