DOGO ASLAY AWAPOLOMOSHEA MJENGO WAZAZI WAKE

MSANII anayekuja kwa kasi kunako gemu la muziki wa kizazi kipya Bongo, Aslay isihaka ameanza kuwaporomoshea mjengo wa maana wazazi wake, eneo la Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, Over The Weekend inakujuza.

Akipiga stori na mwandishi wetu, dogo huyo anayesumbua na ngoma zake kama Naenda Kusema na Uwe Nami, alisema ameamua kuwajengea wazazi wake baada ya kuona wananyanyasika sana kwenye nyumba za kupanga,alisema dog Aslay na kumalizi kwa kusema--

“Mungu amenipa kipaji ili niwasaidie wazazi wangu kwa hiyo kila nitakachokipata kwa sasa nitakielekeza kwenye nyumba hiyo iliyopo Gongo la Mboto. Namshukuru sana Mkubwa Fella kwani yeye ndiyo anayenisimamia kisanii na mafanikio haya yamechangiwa naye kwa kiasi kikubwa,” alisema Aslay

Comments