Mahasimu wao hao lakini, bila shaka, ‘salamu spesho’ toka kwa Cristiano Ronaldo zimeshafika huko Nou Camp baada ya jana Supastaa huyo kuitoa Real nyuma kwa Bao moja na kupiga hetitriki iliyoiwezesha Real kuikung’uta Deportivo La Coruna bao 5-1.
Real, wakitawala, walijikuta wako nyuma katika Dakika ya 16 baada ya Riki kuifungia Deportivo bao.
Lakini Real walizinduka na kupiga bao 3 kabla Haftaimu kwa bao za Ronaldo. Bao mbili, na Di Maria.
Kipindi cha Pili Ronaldo aliongeza moja na Pepe kupiga jingine.
Ushindi huo umewafanya Real wachupe hadi nafasi ya 6 wakiwa na Pointi 10 kwa Mechi 6.
Serie A
Edinson Cavani, baada ya kupiga hetriki
hapo Jumatano dhidi ya Lazio, jana alifunga Penati ya Kipindi cha Pili
na kuipa Napoli ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya Sampdoria na kuifuta rekodi
ya Timu hiyo ya kutofungwa Msimu huu.
Ushindi huu wa Napoli umewafanya
wafungane Pointi na Mabingwa Juventus, ambao Jumamosiwaliwatandika AS
Roma 4-1, wote wakiwa na Pointi 16 kila mmoja toka Mechi 6.
Kwenye Mechi hiyo na Sampdoria, Kocha wa
Napoli Walter Mazzari alitolewa nje katika Kipindi cha Kwanza kwa Kadi
Nyekundu baada ya kulalamika kwa nini Pedro Obiang hakutolewa nje kwa
Rafu mbaya aliyomfanyia Pablo Cannovaro.
Comments
Post a Comment