WAZIRI PINDA AWAVUA MADARAKA WAKURUGENZI SITA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  amewavua madaraka wakurugenzi sita na kuwateua Kaimu Wakurugenzi sita, wakurugenzi wapya 14 na kuwahamisha 27 kutoka katika vituo vyao

Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na kuonyesha udhaifu katika kutekeleza majukumu, kustaafu, kujaza nafasi zilizo wazi katika Halmashauri mpya zilizoanzishwa hivi karibuni na wengine kubadilishiwa majukumu na kurejeshwa katika kazi zao za awali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia akitangaza Wakurugenzi hao na maeneno waliyotoka kwenye mabano ni Willy Njau (DC Mwanga ) aliomba kurejeshwa katika majukumu yake ya awali kutokana na sababu za kiafya, Mpangalukela Tatala (DC Geita), kushindwa kusimamia rasilimaliwatu na fedha, Theonest Nyamhanga (DC Kishapu), kushindwa kusimamia rasilimaliwatu na fedha.

Wengine ni Eden Munisi (DC Morogoro), kuisababishia Halmashauri kupata hati chafu na kushindwa kusimamia rasilimali pamoja na uzembe,  Mhando Senyagwa (DC Kyela), kuwa na kesi mahakamani, Nicholaus Kileka (DC Ngorogoro), alikuwa na kesi inayoendeshwa na Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana Rushwa (Takukuru).

Wakurugenzi wapya walioteuliwa kujaza nafasi zilizo wazi ni Abdallah Kindwanka, aliyekuwa Afisa Ardhi na Wilaya ya Mufindi ambaye  amehamishiwa Geita  kama Kaimu.

Wengine ni Ritius Bilakwata aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Kishapu, kuteuliwa kama  Kaimu wilaya hiyo, aliyekuwa  Mkurugenzi wa Wilaya ya Mpanda, Naomi Nko amehamishiwa Wilaya ya Magu, aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Ukerewe, Abdallah  Mfaume, amehamishiwa Kyela kushika nafasi hiyo.

Aidha aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Monduli, Twalib  Mbasha, ameteuliwa kukaimu nafasi hiyo wilaya hiyo, aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Urambo, Henry Ruyagu, ameteuliwa kukaimu nafasi hiyo wilaya hiyo na Adam Mgowi, aliyekuwa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali amekuwa Mkurugenzi  wa Wilaya ya Mbarali.

Wengine ni Estomih Chang’a aliyekuwa Manispaa ya Arusha na Kaimu Mkurugezi wa Wilaya amepelekwa Wilaya ya  Mpanda kuwa Mkurugenzi, aliyekuwa Mkurugenzi wa Kibaha, Leti Shuma amehamishiwa Wilaya ya Mwanga kwa nafasi hiyo na  aliyekuwa Mkurugenzi wa Kilosa, Mohamed Maje amepelekwa Wilaya ya Namtumbo kwa nafasi hiyo.

Fulgency Mponji  aliyekuwa Afisa Wilaya wa Manispaa ya Songea amepelekwa Moshi  kuwa Mkurugenzi, aliyekuwa Mkurugenzi wa  Njombe, Robert Nehata amehamishiwa Wilaya ya Tunduru kwa nafasi hiyo, Isabela  Chilumba amekuwa Mkurugenzi Wilaya ya  Kahama.

Aidha, aliyekuwa Mkurugenzi wa Kilombero, Fikiri Malembeka amepelekwa Wilaya ya Sengerema kwa nafasi hiyo, aliyekuwa Mkurugenzi wa Tandahimba, Isabela  Chiluba amepelekwa Wilaya ya Ulanga  kwa nafasi hiyo na aliyekuwa  Mkurugenzi wa Wilaya ya  Mufindi, Nasib Mbaga, amehamishiwa Biharamulo kwa nafasi hiyo.

Aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya  Nzega, Idd Nganya, amepelekwa Makete kwa nafasi hiyo,  Jovin Jungu,  aliyekuwa TC Masasi amepelekwa Wilaya ya Chamwino kuwa Mkurugenzi, aliyekuwa Manispaa Iringa, Paul Malala amepelekwa Wilaya ya Njombe kuwa Mkurugenzi  na aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Bukoba, Felix Mabada, amepelekwa Hanang kwa nafasi hiyo hiyo.

Wakurugenzi waliohamishwa ili kujaza vituo wazi ni pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kilindi, Bibie Mnyamagola amepelekwa Kongwa kwa nafasi hiyo, Daudi Mayeji aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Chamwino amepelekwa Kilindi kwa nafasi hiyo hiyo.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Igunga, Protace Magayane, amepelekwa Wilaya ya Nkasi na aliyekuwa Nkasi, Saada Mwaruka amehamishiwa Wilaya ya Mkuranga.

Aidha, Sipora Liana aliyekuwa Mkurugenzi Wilaya ya Mkuranga  amepelekwa Tabora na aliyekuwa Tabora, Hadija Makuwani ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Wilaya ya Tabora.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya Tabora, Doroth  Rwiza amepelekwa Wilaya ya Kasulu kwa nafasi hiyo na aliyekuwa Mkurugenzi wa Kasulu, Kelvin Makonda, amepelekwa Wilaya ya Lindi kwa nafasi hiyo hiyo.

Mkurugenzi wa wa Wilaya ya Ulanga, Pudenciana Kisaka amepelekwa Wilaya ya Iringa , aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya  Iringa, Tina Sekambo amepelekwa Makambako.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Bukoba Beatrice Dominic amepelekwa Wilaya ya Masasi kwa nafasi hiyo, Gladyness Ndyamvuye aliyekuwa  Mkurugenzi Wilaya ya Masasi amepelekwa Wilaya ya Bukoba.

Mkurungenzi wa Wilaya ya Musoma, Nathan Mshana, amepelekwa Wilaya ya Ngorongoro kwa nafasi hiyo, Mkurugenzi wa Wilaya ya Magu, Cornel Ngundungi, amepelekwa Wilaya ya Ngara kwa nafasi hiyo.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Njombe, Mohamed Mkupete amepelekwa Manispaa ya Mtwara, Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro, Dk Koroine Ole Kuney amepelekwa Wilaya ya Misungwi na Mkurugenzi wa Wilaya ya Tunduru, Ephraem Ole Nguyaine amepelekwa Wilaya ya Rorya.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Hanang, Goody Pamba amepelekwa Wilaya ya Igunga kwa nafasi hiyo, Mkurugenzi wa Wilaya ya Tarime, Fidelis Lumato, amepelekwa Wilaya ya Ludewa.

Aidha,  Mkurugenzi wa Wilaya ya Kongwa, Athmani  Akalama amehamishiwa Wilaya ya Tarime na Mkurugenzi wa Mji wa Lindi, Ahmad  Sawa  amepelekwa Halmashauri ya Musoma.

Wakurugenzi waliohamishwa kwenda kwenye Halmashauri Mpya ni  aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara, Magreth Nakainga amepelekwa Geita, Mkurugenzi wa Wilaya ya Wilaya ya Kahama, Eliza Bwana amepelekwa Bariadi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Biharamulo, Zuberi Mbyana  amepelekwa Ilemela, Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Mohamed Nanyanje amepeleka Masasi, Mkurugenzi wa Wilaya ya Sengerema, Erica Musika amepelekwa Kahama na Mkurugenzi wa Wilaya ya Makete, Imelda Ishuza amepelekwa Wilaya ya Busokelo.

Hata hivyo Waziri Ghasia alisema Serikali haitasita kuchukua hatua pale inapobidi ili kuboresha  utendaji kazi na kuwafanya watumishi wawajibike katika majukumu yao ipasavyo.

Comments