
“Baada ya kupatwa ugonjwa huu, Chuz ambaye nilifanya naye kazi kwa usahihi kwenye Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu ambayo kwa sasa ipo madukani, alifika kunijulia hali mara moja tu, tena kwa sekunde chache kisha akaondoka na hajawahi kurudi tena,” alisema kwa masikitiko mzee huyo.
Chuz alipopatikana kwa njia ya simu yake ya kiganjani, alikuwa na haya ya kusema: “Sijamsusa Mzee Kankaa, namheshimu sana tatizo mambo yalikuwa mengi ndiyo maana nikashindwa kwenda kumuona tena, lakini nitakwenda.”
Comments
Post a Comment