Skip to main content
MENEJA NEW CASTLE AFUNGIWA MECHI MBILI
Meneja wa Newcastle Alan Pardew
amefungiwa na Chama cha Soka England, FA, Mechi mbili na kupigwa Faini
ya Pauni 20,000 baada ya kukubali kosa la utovu wa nidhamu kufuatia
tukio kwenye Mechi ya Agosti 18 Newcastle walipocheza na kuifunga
Tottenham bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
Katika Mechi hiyo, Alan Pardew
aliondolewa kwenye Benchi la Ufundi kwa Kadi Nyekundu na Refa Peter
Kirkup alipolalamikia kuwa mpira umetoka nje na kwa ghadhabu akamsukuma
Refa Msaidizi.
Adhabu hii ya Pardew inaanza mara moja
na atalazimika kukaa kwenye Jukwaa la Mashabiki Newcastle watakapocheza
na Everton na kufuatia Mechi na Norwich City kwenye Mechi za Ligi Kuu.
Comments
Post a Comment