MAANDAMANO YA KUDAI AMANI YAFANYIKA UKO MASHARIKI MWA LIBYA

Maandamano ya kupinga wapiganaji mjini BenghaziMaelfu ya Walibya wamefanya mhadhara katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya, kuunga mkono demokrasi na kuwapinga wapiganaji wa Kiislamu.
Waandamanaji waliisihi serikali ya Libya iyapige marufuku makundi ya wapiganaji ambao wamekataa kukabidhi silaha zao tangu vita dhidi ya Kanali Gaddafi mwaka jana.
Waandamanaji wanataka serikali izidishe jeshi na polisi, na walimsifu balozi wa Marekani aliyeuliwa mjini humo juma lilopita.
Waliimba wakati wakiandamana kuelekea medani kuu ya Benghazi.
Muandamanaji mmoja, Faisla al-Naas, alieleza sababu zao:
"Sisi tunaandamana kupinga kundi lenye silaha ambalo halidhibitiwi na serikali.
Wapiganaji hawa wanafaa kujiunga na serikali ili watu wakae kwa salama.
Nchi yetu imekuwa na mtafaruku."
Maandamano mengine ya kuunga mkono wapiganaji yalikuwa madogo sana.

Comments