JESHI LA SUDAN KUSIN LASHAMBULIA NA KUZAMISHA MELI YAO

Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini Kanali Philip AguerWakuu wa Sudan Kusini wanachunguza sababu ya jeshi kushambulia na kuizamisha meli yao wenyewe kwenye Mto Nile.

Wanajeshi kumi walifariki na wengine hamsini wametoweka.
Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini, Kanali Philip Aguer, amesema meli hiyo ilipita kituo cha ukaguzi usiku bila ya kusimama ingawa ilitakiwa kusimama.
Alisema meli hiyo ilikuwa imebeba wanajeshi kama 170.

Comments