Skip to main content
CHINA YAAHIDI KUKUZA UCHUMI ZAIDI
Rais Hu Jintao wa Uchina
ameahidi kuendelea kukuza uchumi wa nchi yake, ili kusaidia kufufua
uchumi wa dunia. Uchumi wa Uchina ni wa pili kwa ukubwa duniani.Bwana Hu aliahidi kwenye mkutano wa viongozi
wa nchi za Jumuia ya Asia-Pacific, unaofanyika mjini Vladivostok
Urusi, kwamba Uchina itafuata sera za kupangilia na itajaribu kuzidisha
soko la ndani ya nchi. Amesema pia kuwa mataifa yote ya eneo hilo nayo
yana jukumu la kuendeleza amani na utulivu.
"Mabibi na Mabwana, uchumi wa dunia uko katika
hali tete, na kazi muhimu sasa, ni kufumbua matatizo na kufanikiwa
kuchangamsha uchumi ili uendelee kukua.
Kuendeleza shime na utulivu
pamoja na kukuza uchumi katika eneo la Pacific ni kwa maslahi ya nchi
zote za kanda hii, na pia ni jukumu letu sote." Alisema.
Naye Waziri Mkuu wa Australia, Julia Gillard,
ilibidi aondoke kwenye mkutano huo kurejea nyumbani, kwa sababu amefiwa
na baba yake, John Gillard, aliyekuwa na umri wa miaka 93.
Comments
Post a Comment