BINGWA WA UEFA CHAMPION NA BINGWA WA EUROPA(CHELSEA V/S ATLETICO MADRID

        >>UWANJA: Stade Louis II, Monaco SAA: 3 Dak 45 Usiku
Miaka 14 iliyopita, katika Mechi ya kwanza ya UEFA SUPER CUP kuchezwa ndani ya Stade Louis II, Monaco, Kiungo wa Chelsea alikuwa Roberto Di Matteo na walitwaa Kombe hilo kwa kuifunga Real Madrid Bao 1-0 na leo hii, Roberto Di Matteo, anaiongoza Chelsea kama Meneja wake akiwania kutwaa tena Taji hilo ambalo linashindaniwa Stade Louis II kwa mara ya mwisho.

UEFA SUPER CUP hushindaniwa kila Mwaka, kabla tu ya hatua za Makundi za CHAMPIONZ LIGI na EUROPA LIGI kuchezwa, na hugombewa na Bingwa wa CHAMPIONZ LIGI, safari hii ni Chelsea, na Bingwa wa EUROPA LIGI, ambae mara hii ni Atletico Madrid.TORRES12
Di Matteo ameahidi kulibeba Kombe na kulirudisha Stamford Bridge.
Msimu huu, Chelsea kama vile wapinzani wao Atletico Madrid, wameuanza vizuri kwa ushindi kwenye Ligi zao lakini Di Matteo amesema: “Nafurahi na mwanzo mzuri na jinsi Wachezaji wanavyocheza. Lakini bado kuna haja ya kujiboresha zaidi.”
Atletico wao walitwaa UEFA SUPER CUP Miaka miwili iliyopita lakini Kocha wao Diego Simeone amesema Chelsea ndio wenye nafasi kubwa kushinda.
Hata hivyo, historia ya UEFA SUPER CUP inaonyesha tangu Mwaka 2000 ni Timu 5 tu kati ya 12 zilizotwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI ndio zimefanikiwa kutwaa Kombe hili.
Wachezaji
FALCAOKwa Straika wa Chelsea, Fernando Torres, Mechi hii ni kama kurudi nyumbani.
Torres, Mika 28, alijizolea sifa akiwa na Atletico ambako aliifungia Bao 82.
Nahodha wa Chelsea, John Terry, ataikosa Mechi hii kwa vile yupo kifungoni kufuatia kutolewa kwake kwa Kadi Nyekundu wakati Chelsea ilipocheza na Barcelona Msimu uliopita na mbadala wake anaweza kuwa Mbrazil David Luis.
Tegemezi kubwa la Atletico ni Straika wao hatari Falcao ambae ndie mashine yao ya magoli.

Comments